bbc.co.uk navigation

Sahel yahitaji msaada zaidi

Imebadilishwa: 19 Februari, 2012 - Saa 16:21 GMT

Umoja wa Mataifa umeonya kuwa baada ya ombi lake la msaada kwa ajili ya Niger, umepata asili-mia-10 tu ya lengo lake, huku ukame na njaa inaendelea kuathiri watu milioni-12 katika kanda yote ya Sahel.

Ukame nchini mali

Akizungumza mjini Agadez, kasjkazini mwa Niger, Helen Clark, wa shirika moja la msaada la Umoja wa Mataifa, aliiambia BBC kwamba ameona watoto wanatapia mlo vibaya na akina mama dhaifu sana.

Umoja wa Mataifa umeomba dola 700-milioni kuweza kukidhi mahitaji ya eneo hilo.

Nchi kadha, kutoka Mauritania hadi Chad zimekumbwa na ukame, na watu wengi wanahama vijiji vyao, kutafuta msaada mijini.

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.