bbc.co.uk navigation

Wala kobe watafukuzwa Zimbabwe

Imebadilishwa: 18 Februari, 2012 - Saa 15:37 GMT

Raia wane wa Uchina wanakabili amri ya kufukuzwa Zimbabwe, baada ya kukamatwa kwa sababu waliwauwa na kuwala kobe adimu.

Mchina alioko Afrika

Wakuu wanaohusika na wanyama, wanasema Wachina hao wamekiri mashtaka ya kuwafanyia ukatili wanyama hao.

Wachunguzi wanasema walikuta magamba ya kobe 40, aina ya Bell's Hinge - aina adimu ya kobe.

Piya walipoingia ndani ya nyumba ya wanaume hao wa Kichina, walikuta kobe wengine 13 kwenye mapipa, wamewekwa bila ya kupewa maji au chakula.

Kobe hao hutumbukizwa ndani ya maji yanayochemka, wakiwa hai.

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.