bbc.co.uk navigation

Umoja wa Mataifa waombwa usaidie Syria

Imebadilishwa: 12 Februari, 2012 - Saa 19:09 GMT

Jumuia ya nchi za Kiarabu imeamua kuuomba Umoja wa Mataifa uisaidie kuunda ujumbe wa amani wa pamoja, kuutuma Syria, ili kumaliza ghasia nchini humo.

Nabil El-Araby, Katibu Mkuu wa Jumuia ya Nchi za Kiarabu

Uamuzi huo ulifikiwa katika mkutano wa jumuia hiyo, unaofanywa Cairo.

Piya mawaziri walikubali kusitisha uhusiano wa kibalozi na Syria, na kuanza mazungumzo na upinzani wa Syria.

Mkuu wa Jumuia ya Nchi za Kiarabu, Nabil El-Araby, aliuambia mkutano kwamba wakati umefika kuchukua hatua thabiti kumaliza adhabu za watu wa Syria.

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.