bbc.co.uk navigation

Ajali yauwa mshauri wa Kabila

Imebadilishwa: 12 Februari, 2012 - Saa 17:28 GMT

Mshauri mwandamizi wa Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, amekufa kwenye ajali ya ndege.

Rais Joseph Kabila

Mshauri huyo, Augustin Katumba Mwanke, alikufa pamoja na rubani, wakati ndege hiyo ya kibinafsi ilipuanguka karibu na mji wa Bukavu, kusini mwa nchi.

Waziri wa Fedha, Augustin Matata Ponyo, na abiria wengine walijeruhiwa vibaya.

Augustin Matata Ponyo, gavana wa Kivu Kusini, Marcellin Cishambo Rohuya, na mshauri mwengine wa rais, Antoine Ghonda, inaarifiwa waliumia vibaya.

Ndege hiyo ilikuwa inasafiri kutoka Kinshasa kuelekea Kivu.

Sababu ya ajali hiyo haijulikani.

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.