bbc.co.uk navigation

Sudan na Sudan Kusini zakutana Addis

Imebadilishwa: 10 Februari, 2012 - Saa 09:32 GMT
Mafuta Sudan Kusini

Mafuta Sudan Kusini

Sudan na Sudan Kusini zitarejea katika mazungumzo mjini Addis Ababa, Ethiopia, leo.

Nchi hizo mbili zimekuwa katika mzozo uliosababishwa na mapato ya mafuta na kwa sehemu ya uamuzi wa Sudan Kusini kusitisha uzalishaji wa mafuta yake.

Sudan Kusini ilipata uhuru wake kutoka Sudan, Khartoum mwezi Julai mwaka jana, huku masuala mengi yanayozihusu nchi mbili hizo jirani yakiwa hayajapatiwa ufumbuzi.

Mwezi uliopita, Sudan Kusini ilifunga uzalishaji wa mafuta yake, baada ya kuishtumu Sudan kaskazini kuiba mafuta hayo.

Sudan kusini ilikuwa ikisafirisha nje mafuta yake hayo kupitia bomba la jirani yake Sudan kaskazini, lakini hapakuwa na makubaliano yoyote kuhusu ushuru wa kupitishia mafuta hayo.

Wanaharakati wa shirika la Global Witness wametaka Muungano wa Afrika, China na serikali za magharibi kuzishinikiza Sudan na Sudan kusini kumaliza tofauti zao.

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.