bbc.co.uk navigation

Mitt Romney ashinda Nevada

Imebadilishwa: 5 Februari, 2012 - Saa 17:00 GMT

Mitt Romney ameshinda katika jimbo la Nevada, kwenye mashindano ya kutafuta mgombea wa urais wa chama cha Republican.

Mitt Romney na wafuasi wake Nevada

Juma lilopita alipata kura nyingi za wafuasi wa Republican katika jimbo la Florida.

Huku kura zinahisabiwa, tayari Bwana Romney alipata asili-mia-40 ya kura za wafuasi, na hivo kumshinda mpinzani wake, Newt Gingrich.

Akihutubia wafuasi wake kwenye mkutano mjini Las Vegas, Nevada, Bwana Romney alishambulia uongozi wa Rais Barack Obama:

"Rais Obama anaipa jina baya na kudharau karibu kila sekta ya uchumi wetu.

Lakini mimi ntaifanya Marekani ivutie sana wafanya biashara, wabunifu na wanaounda nafasi za ajira, ili Marekani ifanye kazi tena.

Na tofauti na watu wengine wanaogombea urais, kazi hiyo naijua vizuri."

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.