bbc.co.uk navigation

Uganda kuanza uchimbaji mafuta

Imebadilishwa: 3 Februari, 2012 - Saa 15:24 GMT
Museveni

Rais wa Uganda- nchi hiyo itakuwa na uwezo wa kuzalisha mapipa laki 2 kwa siku

Serikali ya Uganda imetia saini makubaliano ya uzalishaji mafuta na kampuni ya Uingereza ya jijini London, Tullow oil.

Mkataba huo unafungua njia kwa uwekezaji wa dola bilioni 10 katika kiwanda cha kusafisha mafuta na bomba la kusafirisha mafuta yasiyosafishwa.

Tullow oil itauza robo tatu ya eneo lake la ziwa Albert kwa kampuni ya Uchina CNOOC na kampuni ya Ufaransa ya Total.

Mkataba huo una thamani ya dola bilioni 2.9 na unamaliza mvutano na serikali ya Uganda kuhusu kodi katika siku zijazo.

Waziri wa mafuta wa Uganda Irene Muloni amesema Tullow imekubali mabadiliko ya vipengele vya serikali vya "kuimarisha" ambavyo vitajumuishwa katika mkataba wa kutetea kampuni dhidi ya hasara iwapo serikali itabadili sheria za kodi.

Msemaji wa Tullow George Cazenove amesema kampuni imeridhika na vifungu hivyo.

"Ni muhimu kukumbuka kuwa maendeleo ya bonde la Ziwa Albert yatakuwa ya muda mrefu kwa maendeleo ya Uganda kwa miaka mingi - kuna mafuta mengi sana pale," Bw Cazanove ameiambia BBC.

"Kutakuwa na kiwanda cha kusafisha mafuta nchini Uganda na bomba pia."

Hazina ya mafuta na kiwanda cha kusafisha vitakuwa vinatosha kukidhi mahitaji ya Uganda, na pia baadhi ya nchi majirani ikiwemo mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.