Kesi inayomkabili ya ICC
Unahitaji toleo sahihi la Flash Player kucheza sauti/video
Mahakama ya kimataifa ya ICC inatarajiwa kutoa uamuzi wake kuhusu ikiwa washukiwa wakuu sita wa ghasia za baada ya uchaguzi wa Kenya wa mwaka 2007 wana kesi ya kujibu siku ya Jumatatu.
Kuelekea mwishoni mwa mwaka uliopita, majaji katika ICC walisikiliza upande wa mashtaka na pia utetezi kutathmini ikiwa kuna ushahidi wa kutosha wa kuwashtaki washukiwa hao.
Miongoni mwa washukiwa hao ni naibu waziri mkuu Uhuru Kenyatta , na waziri wa zamani William Ruto, ambao wanadhamiria kugombea kiti cha Urais kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Mwandishi wetu aliyopo Nairobi Anne Mawathe amezungumza na Bw Kenyatta kwanza kufahamu hisia zake binafsi hasa katika maisha yake ya kifamilia.
BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.
Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.