-
Miradi ya kutengeneza bustani inatarajiwa kuanza katika vijiji vitatu maeneo ya kaskazini mwa Turkana. Elisabeth anaishi na watoto wake wanane na anaihudumia familia yake mwenyewe tangu mumewe alipofariki. Alisema: "Ninashukuru sana kwa uchungaji lakini wanyama siku hizi hawawezi kuhimili hali. Kukiwa na ukame, wanyama wako hufa nawe unabaki bila kitu. Kama ningeweza kufanya jambo moja basi ningependa niwe na biashara yangu mwenyewe na kuweza kupata kipato."
-
Selina Napete ni mmoja waliofaidika kutokana na mpango huo wa Oxfam: "Inapokuwa hainyeshi vyanzo vya maji hukauka, matunda hayaivi na wanyama hufa. Hakuna kikubwa unachoweza kufanya ili kuishi. Tulikuwa tukila mara moja kwa siku na watoto wangu walikuwa wakilia kwasababu ya njaa. Nilipoanza bustani ya mboga za majani niliweza kuanza kuwalisha wanangu. Naweza kutumia pesa nilizopata kutokana na mauzo ya mboga hizo kuwapeleka shule na kuwanunulia vitabu.
-
John anaishi karibu na kijiji cha Lomekui ziwa Turkana pamoja na wake zake wawili na watoto 10. Kwa asili ni mchungaji lakini amepata tabu wakati wa ukame. Wanyama wake wengi wamekufa, huku akipata tabu ya kuilisha familia yake. John alipewa ngamia wanne na mbuzi 20 kama sehemu ya mpango wa Oxfam. Alisema: Ni changamoto kubwa kuishi hapa na ukame huu, mifugo haitoi chochote siku hizi na sina namna ya kufanya. Nakumbuka nilicheka sana Oxfam waliponipa ngamia. Katika siku za usoni nataka niongeze idadi ya ngamia na mbuzi."




































