Joseph Kabila ashinda urais tena DRC

Imebadilishwa: 9 Disemba, 2011 - Saa 14:47 GMT

Bw Joseph Kabila

Bw Joseph Kabila ametangazwa mshindi wa nafasi ya urais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo muda mfupi uliopita.

Kulingana na tume ya uchaguzi ya nchi hiyo Joseph Kabila ameshinda kwa asilimia 48.95, mpinzani wake mkuu Etienee Thisekedi akiwa na asilimia 32.33 na Vital Khemere naye akipata asilimia 7.74.

Matokeo hayo yalitarajiwa kutoka siku ya Jumanne lakini maafisa walisema matatizo ya kusambaza vifaa katika nchi hiyo kubwa ndio yalisababisha ucheleweshaji huo.

Wakati huo huo usalama umeimarishwa iwapo patatokea ghasia kufuatia madai ya udanganyifu.

Taarifa zinazohusiana

bbc.co.uk navigation

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.