2 Septemba, 2010 - Imetolewa 03:50 GMT

Dawa za serikali huibiwa barani Afrika

Wagonjwa wa Malaria

Wagonjwa wa Malaria

Matokeo ya utafiti umethibitisha kuwa dawa za kutibu ugonjwa wa Malaria, zinazotolewa kwa nchi kadhaa barani Afrika huibiwa na kisha kuuzwa katika hospitali na duka za kuuza dawa za kibinafsi.

kwenye ripoti iliyochapishwa na jarida moja la matibabu, watafiti kutoka Marekani na Uingereza walinunua dawa kutoka miji kumi na moja barani afrika na waligundua kuwa moja kati ya ishirini ilikuwa mali ya zahati na hospitali za serikali.

Wataalamu wengine wamethibitisha kuwa matokea ya utafiti huo ni ya kweli. Zaidi ya watu milioni moja hufa kila mwaka kutokana na ugonjwa wa malaria barani afrika.

bbc.co.uk navigation

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.