BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 12 Novemba, 2009 - Imetolewa 20:59 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Nigeria wawika dhidi ya Uhispania
 
Chipukizi wa Nigeria wamedhihirisha kwamba wakwao hutunzwa baada ya kuitandika Uhispania mabao matatu kwa moja na kuingia fainali za kombe la dunia kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 17.

Nigeria wataonana na Uswisi ambao hapo awali waliitandika Colombia mabao manne kwa bila.

Fainali ni Jumapili 15 Novemba kwenye mji mkuu Abuja.

Wenyeji walionekana wakakamavu tangu mwanzo huku wakishambulia kwa mizinga.

Bahati yao ilisimama kabla ya kipindi cha mapumziko.

Ingawa Wahispania walirejea na ari mpya huku wakimfanyisha kazi kipa wa Nigeria, vishindo vyao viliambukia patupu kila mara.

Mabao ya Nigeria yalifungwa na Stanley Okoro na Sani Emmanuel

Wahispania walipata kituliza jasho kupitia bao la Borja mnamo dakika ya 83.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha