BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 11 Novemba, 2009 - Imetolewa 15:43 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Mchezaji Sudan kuchapwa kwa "unywaji"
 
Mchezaji nyota kutoka Nigeria, Stephen Worgu, anayesakata kabumbu nchini Sudan, amepatikana na hatia ya kunywa pombe, na amehukumiwa adhabu ya kutandikwa bakora.

Worgu anachezea miamba ya Sudan, Al Merreikh, wenye ngome yao huko Omdurman kaskazini mwa nchi hiyo.

Kilevi ni marufuku katika Sudan Kaskazini kunakokaliwa na idadi kubwa ya waislamu, ingawa inaruhusiwa Kusini ambako hakuna idadi kubwa ya waislamu.

Adhabu kwa mshambuliaji huyo hodari bado haijatekelezwa, kwasababu mwanasheria wake amekata rufaa.

Endapo rufaa yake itakataliwa, Worgu atanyukwa bakora 40 na kutakiwa kulipa pauni 250 za Sudan yapata dola za kimarekani 100.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha