|
Harambee Stars wajifua bila kocha
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, iko njia panda na itacheza mechi dhidi ya Nigeria bila kocha wake Antoine Hey, wakati
itakapokuwa ikiwania fursa ya kucheza fainali za kombe la mataifa ya Afrika.
Kocha wao kutoka Ujerumani, Antoine Hey, hatasimamia timu hiyo katika mechi yao siku ya Jumamosi kufuzu kwa kombe la dunia 2010 dhidi ya Super Eagles. Shirikisho la soka Kenya, Football Kenya Limited, (FKL), limesema kuwa Antoine Hey, amekuwa akikosekana katika mazoezi ya timu hiyo kwa kipindi cha siku tatu. Harambee Stars wanatakiwa kuifunga Nigeria mjini Nairobi siku ya Jumamosi na watumai kuwa Msumbiji watachapwa na Tunisia, ili waweze kufuzu kwa kombe la mataifa ya Afrika 2010. Hata hivyo, Super Eagles bado wana uwezeokano wa kupata tiketi ya kwenda Afrika Kusini kwenye kombe la dunia. |
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||