BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 05 Novemba, 2009 - Imetolewa 19:07 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Afisa afukuzwa kazi juu ya Semenya
 
Afisa mmoja mkuu wa riadha nchini Afrika kusini ameachishwa kazi kwa muda kuhusiana na namna alivyoshughulikia kashfa kuhusu jinsia ya mwanariadha Caster Semenya.

Taarifa kutoka kwa kamati ya Olimpiki nchini humo SASCOC inasema Leonard Chuene ambaye ni mkuu wa shirikisho la riadha nchini humo pamoja na wanachama wake wote watachukuliwa hatua za kinidhamu.

Bwana Chuene amekiri kudanganya kuhusu ikiwa ni kweli Semenya alifanyiwa uchunguzi kubaini jinsia yake.

Hata hivyo afisa huyo alikataa kujiuzulu.

Shirikisho la riadha Afrika Kusini lilitoa taarifa ya kuomba radhi kutoka kwa Semenya, familia yake, Rais pamoja na wananchi wote wa Afrika Kusini kwa namna swala la jinsia ya Semenya lilivyoshughulikiwa.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha